-
(0)By : Emmanuel Munasi
Maandazi ya Haiba
KSh275.00Haiba na marafiki zake wanataka kumnunulia Baraka zawadi anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa. Baraka anaishi na nyanya yake ambaye anaugua. Hata hivyo, kina Haiba hawana pesa za kumnunulia Baraka keki na zawadi nyinginezo. Kwa kuwa likizo imeanza, wanaamua kutafuta njia ya kupata pesa. Je, watatumia mbinu gani? Je, wataweza kupata pesa za kutosha kumnunulia Baraka keki na zawadi nyinginezo?
-
(0)By : Zawadi Namukhula
Miembe ya Ajabu
KSh275.00Toma ananunua miche ya miembe. Bela hapendi miembe hiyo lakini Toma anaipanda. Toma anatunza miembe yake vizuri lakini miembe haikui. Mama na Baba wanasema miembe hiyo si ya kawaida. Je, ni miembe ya aina gani?
-
(0)By : Jackson Omondi
Pango la Ajabu
KSh275.00Zuheri anaanguka pangoni anapocheza mwajificho na wenzake. Baba anapoingia ndani ya pango kumwokoa, anapata kisanduku. Baadaye inatangazwa redioni kuwa polisi wanatafuta kisanduku kilichopotea. Ndani yake mna vitu vya thamani. Je, wazazi wa Zuheri watakabidhi polisi kisanduku kile?
-
(0)By : Daniel Mwangi
Maria Taabani
KSh250.00Maria ana mazoea ya kulala hadi Mama amwamshe. Maria pia husahau kufanya kazi zake za shule hadi Mama amkumbushe. Mama anaenda safari ya mbali. Chacha ambaye ni kakake Maria anataka kumfunza Maria adabu kwa kukosa kumtii. Je, Maria atafanya nini ili asijipate taabani?
-
(0)By : Daniel Mwangi
Ali Apigania Haki Yake
KSh250.00Ali, mvulana mwenye umri wa miaka kumi, anatamani kusoma hadi chuo kikuu. Hata hivyo, nyanya yake anamwagiza kumchungia mbuzi badala ya kwenda shuleni. Ali anabuni mbinu za kurejea shuleni na wakati huo huo kuendelea kumsaidia nyanya yake. Je, juhudi zake zitazaa matunda?
-
(0)By : Jackson Omondi
Tito Anatamani Kuchora
KSh225.00Tito hana vidole. Hata hivyo, ana ndoto ya kufanya kazi ya kuchora na kupaka rangi kama wazazi wake. Siku moja, mwalimu anawaambia wachore wanyama wapendao. Je, Tito atawezaje kuchora bila vidole?
-
(0)By : Zawadi Namukhula
Dereva wa gari Jekundu
KSh225.00Toma na Bella wanataka kwenda shuleni. Wanaona gari jekundu karibu na nyumbani kwao. Dereva wa gari hilo anajitolea kuwapeleka shuleni. Je, dereva ana nia gani? Je, Toma na Bella watakubali awapeleke shuleni?







