-
(0)By : Rosalind Kariuki
K.C.S.E Made Familiar – ENGLISH
KSh735.00This Made Familiar revision book for the Kenya Certificate of Secondary Education (K.C.S.E.) is designed to help students familiarize themselves with K.C.S.E. English questions.
K.C.S.E. English questions that have been tested from 2000 to date.
The questions have been arranged in sections which run across Form 1 to Form 4. The questions in this revision book are in their original form, that is, as they appeared in the K.C.S.E, paper. Beneath every question, the following have been clearly indicated:
* Marks carried by the question,
- Year tested,
- Paper tested in, and % Number in the paper.
Answers at the back of this workbook will allow for performance evaluation after every question.
The change of the syllabus in English though credible, has occasionally thrown the students into a quagmire. Many students have been groping in the dark in their endeavor to handle different questions and frequently learners of a very high capability have been performing dismally.
This book is aimed at inculcating the learner with effective skills of writing description, analysis, synthesis and evaluation in line with Blooms taxonomy. This book will go a long way to acquaint the learners with appropriate skills which will act as a springing board to success.
The contents in the book will surely enable the learners to identify the chronological sequence of ideas given that this will go a long way to give precision in the learners work and help cultivate a positive attitude to English.
Earlier on the English papers captured the various contents differently. Only Poetry, Oral Literature, Compositions and Grammar have been captured between 2000 and 2005.
-
(0)By : Caroline Njenga
K.C.S.E Made Familiar – MATHEMATICS
KSh735.00This mathematics Kenya Certificate of Secondary Education (K.C.S.E.) workbook by Made Familiar Publishers is designed to help students familiarize themselves with K.C.S.E. Mathematics questions – both Paper 1 and Paper 2. The workbook covers past Mathematics questions that have been tested from 1995 to date.
This workbook covers the Alternative ‘A’ syllabus. The questions have been arranged in topics and in their respective forms in which they are taught. Some topics are introduced in one form and wound up in another. The workbook has arranged the questions in these topics as they are taught, and thus appear twice. For example – STATISTICS I (Form 2);
STATISTICS II (Form 4).
The questions in this workbook are in their original form, that is, as they appeared in the K.C.S.E. paper. Beneath every question, the following have been clearly indicated:
- Marks carried by the question,
- Year tested,
- Paper tested in, and
- Number in the paper.
This information will help the students identify topics that are frequently tested and the various ways in which concepts in these topics are tested. Questions that require application of mathematical concepts with general knowledge could not be classified under any topic and have been grouped under ‘mixed concepts’.
Solutions to the questions have been presented at the back of this workbook, and have been calculated to 4 significant figures, unless the question states otherwise.
-
(0)By : Alex Kinyua
Mashujaa wa Korona
KSh350.00Shule zinapofungwa kwa likizo ndefu kutokana na mlipuko wa Ugonjwa wa Korona, Kasala na wenzake wanaamua kushiriki katika mchezo wa kandanda kwenye uwanja wa kuchezea mtaani. Hata hivyo, uwanja huo unafungwa kuzuia kuenea kwa Ugonjwa wa Korona. Wanaamua kushiriki katika miradi mbalimbali. Shule zinapofunguliwa baada ya chanjo ya Korona kuvumbuliwa, kina Kasala wanapata umaarufu shuleni kutokana na mradi walioanzisha katika msimu wa likizo ndefu ya Korona. Je, ni mradi gani huu ambao umewafanya kutawazwa kama mashujaa?
-
(0)By : Orpha Ramogi
Wendi Aokoa Jahazi
KSh350.00Wendi amepewa fursa ya kushiriki katika mchezo wa kuigiza utakaoandaliwa siku ya wazazi shuleni. Lakini anaogopa kuigiza mbele ya watu. Anajiambia kuwa hawezi kushika mistari ya wahusika. Badala yake, anaamua kupamba jukwaa la maigizo. Siku chache kabla ya maigizo kuandaliwa, mhusika mkuu anapata ajali. Bila mhusika huyu, mchezo hautaandaliwa. Je, Wendi atafanya nini ili kuwaokoa wenzake? Je, ataweza kujiamini na kupata ujasiri wa kuchukua nafasi ya mhusika mkuu na kuigiza mbele ya watu?
-
(0)By : Ali Attas
Masaibu ya Juma na Bintiheri
KSh325.00Mapumziko ya Agosti yanakaribia. Mwalimu Kibahaluli anawaambia wanafunzi wake kuwa wazazi wao wamewaandalia ziara ya kukata na shoka. Ziara hiyo haitakuwa ya kiburudani tu bali pia itawafaa katika kupata majibu ya chemshabongo atakayowapa. Juma, Bintiheri na wanafunzi wenzao wanasubiri likizo ya Agosti kwa hamu na ghamu. Je, Mwalimu Kibahaluli atawapa chemshabongo gani mara hii? Je, safari hiyo itawapeleka wapi?
-
(0)By : Nicholas Ogal
Mashujaa wa Mazingira
KSh325.00Mazingira yamejaa aina mbalimbali za taka. Baadhi ya watu wanapata ajali zinazotokana na taka hizi kama vile kukatwa na chupa. Jerry, Tinda na wenzao wanatafuta suluhisho. Je, watafanya nini?
-
(0)By : Ali Attas
Sakata za Juma na Bintiheri
KSh325.00Juma na Bintiheri, ambao ni binamu, pamoja na rafiki yao Lulu wanapofanya utafiti kuhusu kazi waliyopewa shuleni, wanavumbua njia kadhaa za kujipatia mapato. Je, wazazi na walimu wao watakubali na kuwekeza katika uvumbuzi wao?
-
(0)By : Orpha Ramogi
Wakulima Chipukizi na Hadithi Nyingine
KSh300.00Huu ni mkusanyiko wa hadithi fupi fupi zenye matukio ya kuelimisha na kusisimua. Zinajumuisha wahusika chipukizi wanaotumia ujuzi na umilisi waliojifunza darasani pamoja na vipawa vyao kutatua changamoto mbalimbali na kuleta mabadiliko mazuri katika jamii.
-
(0)By : Joe Mirungu
Kitendawili cha Taji na Hadithi Nyingine
KSh300.00Taji na Zalika ni watoto wanaopenda kutunza mazingira yao na kudadisi mambo. Wanashiriki katika visa tofauti tofauti vya kusisimua vinavyowawezesha kutambua na kujifunza mengi kuhusu wanyama na mimea mbalimbali.
-
(0)By : Ali Attas
Ndoto za Juma na Bintiheri
KSh300.00Juma na Bintiheri, ambao ni binamu, wanafunga safari ya Mbuga ya Wanyama ya Tsavo West na Mzima Springs pamoja na wazazi wao. Wanayoshuhudia na kujifunza katika ziara hiyo yanachochea ndoto zao kuhusu kutunza mazingira na kuishi vyema na wanyama wa porini. Pia, yanawafunulia kichemshabongo walichopewa shuleni na mwalimu Kibahaluli. Je, watapata majibu sahihi ya kichemshabongo hicho na kuibuka wanafunzi bora shuleni kwa ubunifu? Jiunge na Juma na Bintiheri katika safari hii ya kiuhalisia na kifantasia iliyojaa vitushi, patashika, mafunzo na vichekesho kwa kusoma hadithi hii ya kusisimua.
-
(0)By : Emmanuel Munasi
Maandazi ya Haiba
KSh275.00Haiba na marafiki zake wanataka kumnunulia Baraka zawadi anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa. Baraka anaishi na nyanya yake ambaye anaugua. Hata hivyo, kina Haiba hawana pesa za kumnunulia Baraka keki na zawadi nyinginezo. Kwa kuwa likizo imeanza, wanaamua kutafuta njia ya kupata pesa. Je, watatumia mbinu gani? Je, wataweza kupata pesa za kutosha kumnunulia Baraka keki na zawadi nyinginezo?
-
(0)By : Zawadi Namukhula
Miembe ya Ajabu
KSh275.00Toma ananunua miche ya miembe. Bela hapendi miembe hiyo lakini Toma anaipanda. Toma anatunza miembe yake vizuri lakini miembe haikui. Mama na Baba wanasema miembe hiyo si ya kawaida. Je, ni miembe ya aina gani?
-
(0)By : Jackson Omondi
Pango la Ajabu
KSh275.00Zuheri anaanguka pangoni anapocheza mwajificho na wenzake. Baba anapoingia ndani ya pango kumwokoa, anapata kisanduku. Baadaye inatangazwa redioni kuwa polisi wanatafuta kisanduku kilichopotea. Ndani yake mna vitu vya thamani. Je, wazazi wa Zuheri watakabidhi polisi kisanduku kile?
-
(0)By : Daniel Mwangi
Maria Taabani
KSh250.00Maria ana mazoea ya kulala hadi Mama amwamshe. Maria pia husahau kufanya kazi zake za shule hadi Mama amkumbushe. Mama anaenda safari ya mbali. Chacha ambaye ni kakake Maria anataka kumfunza Maria adabu kwa kukosa kumtii. Je, Maria atafanya nini ili asijipate taabani?
-
(0)By : Daniel Mwangi
Ali Apigania Haki Yake
KSh250.00Ali, mvulana mwenye umri wa miaka kumi, anatamani kusoma hadi chuo kikuu. Hata hivyo, nyanya yake anamwagiza kumchungia mbuzi badala ya kwenda shuleni. Ali anabuni mbinu za kurejea shuleni na wakati huo huo kuendelea kumsaidia nyanya yake. Je, juhudi zake zitazaa matunda?
-
(0)By : Jackson Omondi
Tito Anatamani Kuchora
KSh225.00Tito hana vidole. Hata hivyo, ana ndoto ya kufanya kazi ya kuchora na kupaka rangi kama wazazi wake. Siku moja, mwalimu anawaambia wachore wanyama wapendao. Je, Tito atawezaje kuchora bila vidole?
















