Taji na Zalika ni watoto wanaopenda kutunza mazingira yao na kudadisi mambo. Wanashiriki katika visa tofauti tofauti vya kusisimua vinavyowawezesha kutambua na kujifunza mengi kuhusu wanyama na mimea mbalimbali.
Lela and Adili live in a village surrounded by forests and wild animals. They enjoy watching the butterflies and birds until a rich man visits the village. He wants to turn part of the village and forest into a private property. Everyone is in despair, but Lela and Adili decide to fight for their cause. With the help of their teacher, the children create persuasive messages on the need to protect the forest which they hope will reach the Governor and the President. Just how far can they go?
Haiba na marafiki zake wanataka kumnunulia Baraka zawadi anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa. Baraka anaishi na nyanya yake ambaye anaugua. Hata hivyo, kina Haiba hawana pesa za kumnunulia Baraka keki na zawadi nyinginezo. Kwa kuwa likizo imeanza, wanaamua kutafuta njia ya kupata pesa. Je, watatumia mbinu gani? Je, wataweza kupata pesa za kutosha kumnunulia Baraka keki na zawadi nyinginezo?
Maria ana mazoea ya kulala hadi Mama amwamshe. Maria pia husahau kufanya kazi zake za shule hadi Mama amkumbushe. Mama anaenda safari ya mbali. Chacha ambaye ni kakake Maria anataka kumfunza Maria adabu kwa kukosa kumtii. Je, Maria atafanya nini ili asijipate taabani?
Mapumziko ya Agosti yanakaribia. Mwalimu Kibahaluli anawaambia wanafunzi wake kuwa wazazi wao wamewaandalia ziara ya kukata na shoka. Ziara hiyo haitakuwa ya kiburudani tu bali pia itawafaa katika kupata majibu ya chemshabongo atakayowapa. Juma, Bintiheri na wanafunzi wenzao wanasubiri likizo ya Agosti kwa hamu na ghamu. Je, Mwalimu Kibahaluli atawapa chemshabongo gani mara hii? Je, safari hiyo itawapeleka wapi?
Shule zinapofungwa kwa likizo ndefu kutokana na mlipuko wa Ugonjwa wa Korona, Kasala na wenzake wanaamua kushiriki katika mchezo wa kandanda kwenye uwanja wa kuchezea mtaani. Hata hivyo, uwanja huo unafungwa kuzuia kuenea kwa Ugonjwa wa Korona. Wanaamua kushiriki katika miradi mbalimbali. Shule zinapofunguliwa baada ya chanjo ya Korona kuvumbuliwa, kina Kasala wanapata umaarufu shuleni kutokana na mradi walioanzisha katika msimu wa likizo ndefu ya Korona. Je, ni mradi gani huu ambao umewafanya kutawazwa kama mashujaa?
Mazingira yamejaa aina mbalimbali za taka. Baadhi ya watu wanapata ajali zinazotokana na taka hizi kama vile kukatwa na chupa. Jerry, Tinda na wenzao wanatafuta suluhisho. Je, watafanya nini?
Zawadi na Bahati wanapenda kutazama anga. Wanashangaa jinsi rangi ya angani inavyobadilika. Mara ni nyeusi. Mara ina upinde wenye rangi nyingi. Je, mbingu ina rangi gani?
Toma ananunua miche ya miembe. Bela hapendi miembe hiyo lakini Toma anaipanda. Toma anatunza miembe yake vizuri lakini miembe haikui. Mama na Baba wanasema miembe hiyo si ya kawaida. Je, ni miembe ya aina gani?